Amesema mkutano huo unatoa fursa ya kutathmini mafanikio ya utekelezaji wa Ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama, pamoja na kubainisha changamoto na mikakati mipya ya kuimarisha utekelezaji wake barani Afrika.Dkt. Gwajima ameeleza kuwa licha ya hatua nzuri zilizopigwa katika kupanua usawa wa kijinsia, wanawake bado wanakabiliwa na vikwazo mbalimbali huku akitaja mila na desturi kandamizi, changamoto za kiuchumi na athari wanazokutana nazo wanawake wanaojitokeza kugombea nafasi za uongozi kuwa miongoni mwa mambo yanayopunguza ushiriki wao katika uongozi na siasa.
Amesisitiza kuwa utekelezaji wenye tija wa ajenda ya WPS unahitaji ushirikiano mpana kati ya serikali, mashirika ya kiraia, wadau wa maendeleo na taasisi za kikanda huu akisema Tanzania itaendelea kushirikiana na Umoja wa Afrika na wadau wengine ili kuhakikisha wanawake wanapata nafasi stahiki katika meza za maamuzi na michakato ya ujenzi wa amani barani Afrika.
Hata hivyo, ameonya kuwa teknolojia hiyo hiyo imekuwa ikichochea aina mpya za ukatili wa kijinsia mtandaoni, ambao waathirika wakubwa ni wanawake na wasichana.
Amefafanua kuwa mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kusambaza video za uongo, chuki, vitisho na matusi yanayolenga kuwachafua wanawake hadharani, jambo linalotishia usalama wao mtandaoni na kuwavunja moyo wanaotaka kushiriki katika uongozi na siasa.
Aidha amehimiza wadau wote kushiriki kikamilifu katika kutoa hamasa na elimu juu ya matumizi salama ya mitandao ili kulinda wanawake, wasichana na jamii kwa ujumla.

Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership.Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania.
“The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said.
The discussions centred on ongoing negotiations involving major U.S.-linked strategic investments. Both sides acknowledged that talks on two flagship projects—the LNG Project and Tembo Nickel Project—are now in their final stages, pending formal signing. A third investment, the Mahenge Graphite Project, remains under active technical review.
President Samia welcomed Washington’s renewed commitment and assured the delegation that Tanzania remains focused on completing the remaining procedural steps.
“As a non-aligned nation, Tanzania is open, ready, and committed to working with all partners who respect our sovereignty and share our vision for prosperity,” the President said.
“These strategic projects are of national importance, and we are determined to finalise them so they can unlock jobs, investment, and sustainable prosperity for our people.”
The President highlighted that more than 400 American companies currently operate in Tanzania—reflecting the country’s stability, openness to investment, and strong historical ties with the United States.
Beyond investments, the meeting touched on broader areas of cooperation, including political stability, regional security, economic reforms, private-sector growth, health-sector partnerships, and people-to-people exchanges.
Ambassador Lentz congratulated President Samia for her vision and long-term national planning through Vision 2050, noting the U.S. Government’s readiness to support its implementation and reinforce the President’s 4R philosophy of reconciliation, resilience, reforms, and rebuilding trust.
Both sides agreed that strengthened communication, consistent engagement, and timely action on pending agreements are key to unlocking the full potential of U.S.–Tanzania relations.
This meeting marks a pivotal moment in redefining and revitalising the U.S.–Tanzania relationship. The reaffirmed commitment from both governments signals the emergence of a modern, transparent, private-sector-driven partnership rooted in shared prosperity, mutual respect, and long-term strategic cooperation.
Flagship Projects
1. LNG Project — Estimated Value: USD 42 Billion
A transformative natural gas development involving leading international energy companies. The project aims to unlock Tanzania’s vast offshore gas reserves, boost national revenue, create thousands of jobs, and position the country as a major global LNG supplier.
2. Tembo Nickel Project — Value: USD 942 Million
A major critical-minerals investment in Ngara focused on nickel—an essential component in electric-vehicle batteries. The project will support global clean-energy supply chains, stimulate industrialisation, and expand Tanzania’s export base.
3. Mahenge Graphite Project — Value: USD 300 Million
One of the world’s largest high-grade graphite deposits, positioned to serve the fast-growing battery and renewable-energy sectors. The project will reinforce Tanzania’s role as a leading supplier of battery-grade minerals.
Rais Samia ameukaribisha upya msimamo wa Marekani na kuhakikishia ujumbe huo kuwa Tanzania itaendelea kusimamia hatua zote zilizobaki ili kukamilisha taratibu na kufungua njia ya utekelezaji wa miradi hiyo.“Kama taifa lisilofungamana na upande wowote, Tanzania iko wazi, tayari na imejitoa kufanya kazi na washirika wote wanaoheshimu uhuru wetu na kushiriki katika dira yetu ya maendeleo,” alisema Rais.
“Miradi hii ni ya umuhimu mkubwa kwa taifa, na tumejidhatiti kuikamilisha ili iweze kufungua ajira, uwekezaji, na ustawi endelevu kwa wananchi wetu.”
Rais pia alibainisha kuwa zaidi ya kampuni 400 za Marekani kwa sasa zinafanya shughuli zao nchini Tanzania—kiashiria cha uthabiti wa nchi, mazingira mazuri ya uwekezaji na historia ya muda mrefu ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa haya mawili.
Mbali na uwekezaji, mazungumzo yamegusa maeneo mapana ya ushirikiano ikiwemo utulivu wa kisiasa, usalama wa kikanda, mageuzi ya kiuchumi, ukuaji wa sekta binafsi, ushirikiano katika afya na programu za kubadilishana uzoefu kati ya wananchi wa nchi hizi mbili.
Balozi Lentz amempongeza Rais Samia kwa maono na mipango madhubuti ya muda mrefu kupitia Vision 2050, na kusisitiza kuwa Serikali ya Marekani iko tayari kuunga mkono utekelezaji wake pamoja na kuimarisha falsafa ya 4R ya Rais—maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya imani katika utawala.
Pande zote zimekubaliana kuwa mawasiliano ya karibu, ushirikiano wa mara kwa mara, na hatua za haraka katika kukamilisha makubaliano yaliyosalia ni muhimu katika kufungua uwezo kamili wa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani.
Kikao hiki kinawakilisha hatua muhimu katika kufafanua upya na kuhuisha mahusiano kati ya Tanzania na Marekani. Dhamira ya pamoja iliyothibitishwa na serikali zote mbili inaashiria mwanzo wa ushirikiano wa kisasa, wazi, unaoongozwa na sekta binafsi—ukijengwa juu ya ustawi wa pamoja, kuheshimiana na ushirikiano wa muda mrefu wa kimkakati.
Miradi Mikuu ya Kimkakati
1. Mradi wa LNG — Thamani Inayokadiriwa: Dola Bilioni 42
Mradi mkubwa wa kugundua na kuchakata gesi asilia unaohusisha kampuni kubwa za kimataifa za nishati. Mradi huu unalenga kufungua hazina kubwa ya gesi iliyopo baharini, kuongeza mapato ya taifa, kuunda maelfu ya ajira na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia kama mchezaji muhimu wa LNG.
2. Mradi wa Tembo Nickel — Thamani: Dola Milioni 942
Uwekezaji mkubwa wa madini muhimu eneo la Ngara unaolenga nikeli—kiungo muhimu katika utengenezaji wa betri za magari yanayotumia umeme. Mradi huu utaimarisha minyororo ya kimataifa ya nishati safi, kuchochea viwanda na kuongeza pato la mauzo ya nje.
3. Mradi wa Mahenge Graphite — Thamani: Dola Milioni 300
Chanzo kikubwa duniani cha madini ya graphite yenye ubora wa juu, yenye umuhimu katika uzalishaji wa betri na teknolojia za nishati jadidifu. Mradi huu utaimarisha nafasi ya Tanzania kama mtoa huduma mkuu wa malighafi muhimu za viwanda vya kisasa vya betri.












































